Al-Abbas Dental Clinic Bukoba

Al-Abbas Dental Clinic Bukoba TUNATOA HUDUMA ZA KINYWA NA MEMO

DENTAL SERVICES

21/07/2018

TANGAZO

ANAHITAJIKA DAKTARI WA MENO (DT) KTK PRIVATE HOSPITAL BUKOBA MKOA WA KAGERA

AMBAE YUKO TEYARI TAFADHALI WASILIANA NA WAHUSIKA NAMBA 0767291030/0677010050

TAFADHALI SHARE KATIKA GROUP NYINGINE.

TATIZO LA KUSAGA MENO KWA WATOTO WADOGO.Salamu kutoka AL-BBAS DENTA CLINICTunaomba radhi kwa wasomaji wetu, wafuatiliaji...
12/07/2018

TATIZO LA KUSAGA MENO KWA WATOTO WADOGO.

Salamu kutoka AL-BBAS DENTA CLINIC

Tunaomba radhi kwa wasomaji wetu, wafuatiliaji wa makala zetu kwa muda kidogo tulikuwa busy lakini leo tumerudi na makala zetu zitaanza kuja k**a kawaida.

Kichwa cha habari hapo juu kinahusika na somo hili litakujieni katika sehemu ya kwanza na ya pili kisha tutaanza somo lenye kichwa cha habari ( TATIZO LA KUSAGA MENO KWA WATU WAZIMA)

Kila mzazi anatakiwa kufahamu kwamba tatizo tatizo la kusaga meno kwa watoto mara nyingi hujitokeza kwenye mabadiliko ya tabia na mwenendo wa mtoto kwa sababu ya mihemko na mwitikio wake unaomsumbua akiwa amelala usiku.

Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 20 ya watoto kati ya mwaka 1 hadi miaka 11 husumbuliwa na kusaga meno tatizo ambalo kwa kitaalamu linajulikana k**a Bruxism.

Hata hivyo takwimu hii inakadiriwa kuwa chini ya hali halisi kwa vile wazazi wengi wanashindwa kutambua tatizo hili kwa watoto wao.
Dalili za tatizo hili zinafanana kwa karibu na matatizo mengine ya watoto hivyo inawawia vigumu wazazi ama walezi kutambua tatizo hili na kulipuu*ia.

JE TATIZO HILI HASA HUWAPATA WATOTO GAN?

Tatizo hili mara nyingi huwapata watoto wenye shida ya kupumua vizuri hivyo hupumua kwa kutumia mdomo,Watoto walio na vivimbe vya tezi, watoto wenye tatizo la ku*iba kwa njia ya hewa wanapokuwa usingizini na watoto wenye tatizo la meno kuota kwa mpangilio mbaya.

JE WATOTO WENYE MATATIZO YA AKILI NA UTINDIO WA UBONGO WANAPATWA NA TATIZO HILI?

Tukutane tena katika sehemu yetu ya mwisho kwa somo hili.

Kwa ushauri wa kina zaidi kuhusu afya ya kinywa chako na meno tafadhali wasiliana nasi kupitia namba yetu hapo chini

0767291030

Au fika katika AL-Al-Abbas Bukoba Ilioko Uhuru Road karibu na Victoria Hotel au Linas Night Club.

*JINSI YA KUTUNZA MENO YAKO* Unapotizama kwenye kioo, wewe hutazama nini?Labda wewe hutazama nywele zako au sehemu nying...
23/06/2018

*JINSI YA KUTUNZA MENO YAKO*

Unapotizama kwenye kioo, wewe hutazama nini?
Labda wewe hutazama nywele zako au sehemu nyingine ya uso wako.

Lakini Vipi kuhusu meno yako? Je, umetambua kwamba jinsi ambavyo wewe hutabasamu hutegemea hasa meno yako?

Naam, ikiwa unajali tabasamu yako, utatunza meno yako.

*Meno ya mtu mzima yanapaswa kudumu muda wote wa maisha yake*

Yanapaswa kutunzwa vizuri. Mbali na kutafuna chakula na kukusaidia kuzungumza kwa njia nzuri, meno yako hutegemeza midomo na mashavu yako na hivyo kuboresha tabasamu yako na kuifanya ivutie.

*Kwa kweli, meno yako ni muhimu sana!*

https://chat.whatsapp.com/G4ufv4lFfHJEuZ0Xgvf4fy

UGAGA (CALCULUS) Je meno yako yamelegea?Je, meno yako yamepinda, na kuacha nafasi wakati hapo kabla hayakuwa hivyo?Je, J...
22/06/2018

UGAGA (CALCULUS)

Je meno yako yamelegea?

Je, meno yako yamepinda, na kuacha nafasi wakati hapo kabla hayakuwa hivyo?

Je, Je fizi zako zimejivuta chini na kufanya meno yako yaoenekane ni marefu sana.

Je, Fizi zako hutoa damu wakati wa kupigwa mswaki?

Je, unatoa harufu mbaya mdomoni na kupata maumivu ya fizi

Je, Meno yako yanalegea tu na kutoka bila kuoza?

Nafikiri jibu lako ni ndio? K**a huna dalili zote basi una moja kati ya hizo, na k**a zimetimia zote basi hiyo ni tatizo gani?

Hiyo ni UGAGA………KITAALAMU TUNAITA ( CALCULUS )

Ni utando mgumu sana unaojijenga kwenye meno hasa pale ambapo ufizi unaishia .
Tabaka hili linapojijenga na hatimaye kuwa gumu huwa haliwezi kutoka kwa mswaki.

Tafadhali baada ya kusoma ujumbe huu, chukua kiyoo chako ujikague kinywa chako kwa umakini, unaweza kutizama picha tulizoziweka kisha ukafananisha na kinywa chako.

AL-ABBAS DENTAL CLINIC ILIOKO BUKOBA MJINI INATOA HUDUMA KWA WALE WENYE MATATIZO HAYA. TAFADHALI FIKA KATIKA CLINIC YETU KWA MSAADA ZAIDI.

NAMBA ZETU NI +255 767 291 030 unaweza kupiga au kutuma whatsapp msg una utajibiwa.

PAMOJA NA HAYO PIA TUNAFANYA HUDUMA ZIFUATAZO.

Tunang’oa meno

Tunaziba meno yenye matundu.

Tunasafisha kinywa chenye kutoa harufu mbaya

Tunafanya RCT

Tunakaza meno yaliolegea.

Tunasafisha meno kwa mtu alietumia vinywaji venye rangi k**a kahawa na………pia kwa alievuta sigara meno yakabadilika.

Tunaunga taya zilizovunjika kwa ajali

TUNATENGENEZA MENO YA BANDIA.

SAMBAZA UJUMBE HUU, NA LIKE PAGE YETU, TUTAKUTUMIA UJUMBE WA KUPATA NAFASI YA KUONANA NA WATAALAMU WETU BURE KWA UANGALIZI WA MENO YAKO.

AL-ABBAS DENTAL CLINIC

ITS TIME TO SMILE AGAIN.

JE UNASUMBULIWA NA MAUMIVU YA FIZI KUTOKWA NA DAMU, HARUFU MBAYA MDOMONI, NA MENO KUUMA?UGONJWA huu unawapata watu wengi...
10/06/2018

JE UNASUMBULIWA NA MAUMIVU YA FIZI KUTOKWA NA DAMU, HARUFU MBAYA MDOMONI, NA MENO KUUMA?

UGONJWA huu unawapata watu wengi sana ulimwenguni. Hata hivyo, katika hatua za kwanza dalili zake hazionekani haraka. Ugonjwa wa fizi ni hatari kwa kuwa hautambuliki mapema.

Kitabu International Dental Journal kinataja ugonjwa wa fizi kati ya magonjwa ya kinywa yanayosababisha “tatizo kubwa la afya ya umma.” Kinaendelea kusema kwamba ugonjwa wa kinywa “unaweza kusababisha uchungu mwingi na kuteseka na vilevile kupunguza uwezo wa mtu wa kula na kufurahia maisha.”

Kuchunguza ugonjwa huo kunaweza kukusaidia kujikinga.

Taarifa Kuhusu Ugonjwa wa Fizi
Ugonjwa wa fizi una hatua mbalimbali. Hatua ya kwanza ni kuvimba fizi (gingivitis). Fizi zinazotoa damu ni dalili ya hatua hiyo. Huenda mtu akatokwa na damu anapopiga mswaki, au anapotoa uchafu kwenye meno kwa kutumia u*i mwembamba au bila sababu yoyote. Vilevile, kutokwa na damu mtu anapochunguzwa meno na daktari ni dalili ya ugonjwa huo.

Ugonjwa wa fizi husonga kwenye hatua inayofuata (periodontitis). Kufikia hatua hiyo, mifupa na fizi zinazotegemeza meno, huanza kuharibika. Ugonjwa huo wa fizi huenda usiwe na dalili zozote hadi unapokuwa mbaya zaidi.

Dalili fulani za hatua hiyo ni kutokea kwa nafasi kati ya fizi na meno; kulegea kwa meno; mianya kati ya meno; kunuka mdomo; fizi zinazoachana na meno na kufanya meno yaonekane kuwa marefu zaidi; na kutokwa na damu kwenye fizi.

KWA MTU YEYOTE MWENYE UGONJWA WA FIZI AMA TATIZO LOLOTE LA MENO TAFADHALI FIKA KATIKA CLINIC YETU ILIOPO BUKOBA MJINI

KWA MAWASILIANO PIGA NAMBA
0767291030P

PLS SHARE

Address

UGANDA Road
Bukoba
255

Opening Hours

Monday 07:30 - 17:00
Tuesday 07:30 - 17:00
Wednesday 07:30 - 17:00
Thursday 07:30 - 17:00
Friday 07:30 - 17:00
Saturday 07:30 - 03:00
Sunday 07:30 - 12:00

Telephone

+255767291030

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Al-Abbas Dental Clinic Bukoba posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Al-Abbas Dental Clinic Bukoba:

Share